Posts

Showing posts from September, 2017

JINSI YA KUTUMA APK WHATSAPP KWA MTU AU GROUP

Image
Habari! Leo tutajifunza namna ya kutuma APK kwenye group whatsapp au kumtumia mtu binafsi. Kwa wasioelewa maana ya APK maana yake ni file fulani litakalo muwezesha mtu kuinstall application kwenye simu yake. Ili uweze kutuma APK kwa njia ya whatsapp yakupasa kwanza kuwa na hiyo APK kwenye simu yako. Si lazima uidownload hiyo APK bali kama una application husika kwenye simu yako unayohitaji kuituma waweza itengenezea APK yake. Ni kwa jinsi gani nitaitengeneza APK kutoka kwenye APP niliyonayo tayari kwenye simu? 👉Kuna namna nyingi na app nyingi zinazoweza kukusaidia kutengeneza APK kutoka kwenye APP ambayo unayo tayari kwenye simu yako, lakini mimi hapa nitaelekeza kwa kutumia ES File Explorer. 👉ES File Explorer ni APP aminika na pendwa kwa wadau wote wenye maujuzi ya simu hasa ukiwa umeroot simu yako. Hauna haja ya kuwa na APP nyingi kwenye simu yako zenye kufanya kazi ya kujirudia rudia. Mahitaji: • Android phone • Whatsapp app • ES File Explorer app Zingatia:  ...

MAOMBI YAFUNGULIWA TENA KWA WAOMBAJI WA DIPLOMA NA CERTIFICATE MWAKA WA MASOMO 2017/18

Image
NACTE BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI   (NACTE)   TAARIFA KWA UMMA KUHUSU AWAMU YA PILI YA MAOMBI YA UDAHILI KWA WAOMBAJI WA ASTASHAHADA NA STASHAHADA MWAKA WA MASOMO 2017/2018 Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kufahamisha umma kuwa baada ya  kukamilika kwa awamu ya kwanza  ya Udahili, awamu ya pili imefunguliwa kuanzia tarehe  18 Septemba, 2017 hadi tarehe 1 Octoba, 2017  kwa vyuo vyote ambavyo bado vina  nafasi wazi  za udahili.  Hivyo wahitimu wote wa Elimu ya Sekondari wenye sifa za kujiunga na programu za Astashahada na Stashahada, walioomba na hawakufanikiwa kupata nafasi katika  awamu ya kwanza  na wale ambao hawajaomba hadi Udahili ulipofungwa tarehe 20 Agosti, 2017 watume maombi ya Udahili kwenye vyuo vya serikali na binafsi.  Kwa wanaotaka kuomba vyuo vya Serikali/Umma kwa fani za Ualimu na Afya watume maombi yao kwa njia ya...

KOZI ZA NURSE ASSISTANTS NA MEDICAL ATTENDANTS HAZITAMBULIWI NA BARAZA

Image
NACTE BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI     (NACTE)   TAARIFA KWA UMMA Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), linapenda kuwataarifu Wadau wa Elimu na Umma kwa ujumla kwamba mafunzo ya Wauguzi Wasaidizi (Nurse Assistants) na Wahudumu wa Afya (Medical Attendants)  si miongoni mwa mafunzo yanayosimamiwa na kutambuliwa na Baraza , na kwamba chuo chochote kinachotoa na kuendesha mafunzo hayo kinakiuka Kanuni za Usajili pamoja na Kanuni za Ithibati za Baraza za mwaka 2001. Kwa tangazo hili Baraza linawatahadharisha wananchi kwa ujumla kutojiunga na mafunzo yaliyotajwa hapo juu kwa kuwa tuzo zinazotolewa baada ya kuhitimu mafunzo hayo pia hazitambuliwi. Aidha Baraza linaendelea kufuatilia na kuvibaini vyuo vyote vinavyotoa mafunzo hayo kwa ajili ya kuchukua hatua stahiki. Kituo au chuo chochote kitakachokutwa kinatoa mafunzo ya aina hiyo, wahusika watakabidhiwa kwenye vyombo vya Sheria kwa udanganyifu...

NACTE SELECTION RESULTS ARE OUT 2017/18 FIRST BATCH

Image
The Student's Admission Verification for those who expected to join Health and Teacher Government Institutions has been completed, You can view results of this selection from Your Personal profile by clicking  here , The System will open soon for second round to allow new applicants and those who were eligible and not selected to make there new choices. Thank you. 

ALL ABOUT ANDROID ROOTING

Image
INTRODUCTION           On the topic of Android, it is most likely that ROOTING is the keyword that you may comeacross with high frequency when researching "Android". So, you want to know about rooting your Android? This may sound a little bit confusing and maybe scary. It's kind of a big decision to make. To root, or not to root. Let's do not rush and read a little more about its advantages and disadvantages before you root your Android device. About Rooting          Android, as an operating system that is rife in this era of Smartphones, is based on Linux. Anyhow, apps need permission to access certain parts of Linux, and not all of them have this "root" access. Just as other operating systems, the one running on your Android phone is also designed with several limitations and restrictions by carriers or manufacturers for commercial concerns and also safety reasons. ROOTING, on the other hand, is a modification ...

MASWALI NA MAJIBU KWA WAOMBAJI WA MIKOPO KWA 2017/18

Image
Bodi ya mkopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB) imetoa majibu juu ya maswali yote ambayo waombaji wa mkopo huo wamekuwa nayo. Bodi imeamua kuainisha maswali 17 ambayo yamekuwa yakiulizwa mara kwa mara pamoja na majibu yake. Miongoni mwa maswali hayo ni Je! ni wapi nitahakiki cheti cha kuzaliwa au kifo cha mzazi/mlezi? ikiwa ni pamoja na suluhisho la nini cha kufanya kwa wale ambao walituma pasipo kufanya hivyo. Kusoma maswali zaidi BINYA HAPA  kudownload maswali hayo yaliyotumwa kwa mfumo wa pdf. USISITE KUWA UNATEMBELEA BLOG HII KWA UPDATES NYINGINEZO MUHIMU KUHUSU MKOPO NA CHAGUZI ZA VYUO.

TUNDU LISSU AJERUHIWA KWA RISASI DODOMA, AKIMBIZWA HOSPITALI

Image
Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, ajeruhiwa kwa risasi.                   Kwa sasa wapo hospitali ya Mkoa, mjini Dodoma. Ameshambuliwa kwa risasi wakati akishuka nyumbani kwake Area D Mjini Dodoma, alikuwa akitokea Bungeni na alienda Nyumbani kula chakula cha mchana. Lissu amepigwa risasi 5, miguuni na tumboni. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema hali ya Mbunge huyo aliye hospitalini sasa ni mbaya! KUTAZAMA PICHA ZAIDI ZA TUKIO  BINYA HAPA

JINSI YA KUPENDA - 3

Image
Habari! Ni siku nyingine imempendeza Mungu kupata kibali cha kukuandikieni makala hii ya tatu na ya mwisho katika somo letu la JINSI YA KUPENDA. Bila shaka umepata kitu katika mfururizo wa somo hili. Usisahau kwamba dhana ya Upendo inazungumzwa kwa namna nyingi sana ila ni juu yako kulinganisha kizungumziwacho na hali halisi iliyopo. Kama ndio unaungana nasi huwezi pata mtiririko mzuri hivyo ni vyema ukaanza sehemu ya kwanza kwa KUGUSA HAPA Ebu sasa tujikumbushe tulipoishia wakati uliopita, Tuliona kuna njia tano za kupenda kwa vitendo (hii ni kwa kuanzia, waweza gundua mengi zaidi baada ya kuyafanya haya), na tuliona kipengele cha kwanza cha Kutenda vitendo vya ukarimu, leo hii tutaendelea katika vipengele vinne vilivyosalia na kufunga mada hii. Karibu 2. KUZUNGUMZA KWA MANENO YA UPOLE NA KUSHUKURU           Kila mtu anahitaji kuthaminiwa, Sote hupenda kusikia wenza wetu wakizungumza nasi kwa upole na sio kutukaripia. Lakini pia hujisikia vizuri z...

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA WATER INSTITUTE UBUNGO

Image
Kama wewe ni mzazi, mlezi au mwanafunzi miongoni mwa walio omba kusoma ordinary diploma katika chuo cha maji ubungo mwaka wa masomo 2017/2018 basi orodha ya majina ya waliochaguliwa na ambao hawajachaguliwa tayari ilishatolewa. Orodha imetolewa kwa rawamu mbili: Kutazama awamu ya kwanza binya  HAPA Kutazama awamu ya pili binya  HAPA Pia mbali na kuotoa orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa na ambao hawajachaguliwa pia chuo hicho cha maji wametoa Join instruction na kuna fomu ya kujaza na kuipeleka chuoni kwa wale wanaohitaji kupata vyumba chuoni hapo. Kudownload Join instruction binya  HAPA Kudownload fomu ya accommodation binya  HAPA KWA TAARIFA ZA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO USISITE KUWA UNATEMBELEA KATIKA BLOG HII YA superneat2013.blogspot.com USISAHAU KUSHARE NA WENZAKO ILI TAARIFA ZIZIDI KUSAMBAA NA KUWAFIKIA WALENGWA

JINSI YA KUPENDA - 2

Image
JINSI YA KUPENDA            Hebu sasa baada ya utangulizi katika sehemu ya kwanza tulipopata nafasi ya kuangalia maana ya upendo na hisia ya penzi, hivi sasa tuzungumze kwa kina ni kwa njia gani tunaweza kuwapenda wenzi wetu. Kama huku soma makala ya sehemu ya kwanza GUSA HAPA Njia halisi za kupenda kwa vitendo ni: 1. Kutenda vitendo vya ukarimu 2. Kuzungumza kwa maneno ya upole na     kushukuru 3. Kusaidia 4. Kusamehe na kuachilia 5. Kumkubali mwenzio kama alivyo. 1. KUTENDA VITENDO VYA UKARIMU           Kutenda vitendo vya ukarimu ni njia moja wapo ya kupenda. Siku zote mwanzo wa mahusiano kila mtu huwa mwangalifu sana kutenda vitendo vizuri kwa mwenza wake asije mkosea na ndio maana mwanzoni mwa mahusiano yoyote penzi huwa tamu zaidi lakini baada ya muda mrefu wa mahusiano hayo hali hubadilika. Je! unafikiri unapaswa kuacha kufanya vitendo vya ukarimu baada ya muda fulani? hapana hupaswi kuacha kutenda ...

JINSI YA KUPENDA - 1

Image
Utangulizi Habari, leo ni siku njema ambapo tutazungumzia swala zima la jinsi ya kupenda. Pengine umepata mshangao kidogo baada ya kuona kichwa cha habari na kujiuliza: hivi kuna njia maalumu ya kupenda? Usiwe na mashaka nifuatilie kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa makala hii naamini utanielewa vizuri zaidi na utaboresha upendo kwa mweza wako au pengine kama upendo baina yenu wawili ulikuwa umepotea utashangaa kuona mapenzi baina yenu yamerejea na kuongeza furaha katika mahusiano yenu. NB: Kwa matokeo mazuri usisome peke yako share na mwenza wako pia kwa kusoma nae kwa sauti mkipokezana kwa zamu huku mkiwa sehemu tulivu zaidi ambapo yaweza kuwa chumbani, beach au sehemu yoyote ilimradi iwe tulivu au pia kama sio hivyo mtumie link asome makala hii ili na yeye atambue nini cha kufanya. Ili kuelewa jinsi ya kupenda kwanza kabisa lazima utambue maana halisi ya upendo. Je! Umewahi kujiuliza upendo ni nini? Kama jibu ni ndio, ulipata majibu gani kuhusu upendo tafadhali share na mimi kw...